Burudani

Galaxy avutiwa na Mimi Mars

Msanii Galaxy amefunguka kuwa anatamani kufanya kazi na hitmaker wa Dede, Mimi Mars ambaye amekuwa na uwezo mzuri wa kuchezea sauti yake kwenye nyimbo zake.

Muimbaji huyo wa Top In My Heart, ameiambia Bongo5 kuwa japo hajafanya mawasiliano yoyote na uongozi wa msanii huyo lakini anatamani kufanya naye kazi na huwenda akawa ndio msanii wake wa kwanza kwenye Bongo Flava kumshirikisha kwenye nyimbo zake.

“Navutiwa sana kufanya collabo na Mimi Mars. Nimevutiwa na sauti yake kwa kweli, naona kama nikifanya naye kazi itakuwa ngoma kali sana. Sikuwahi kufikiria kufanya kazi mapema hivi na msanii yoyote hapa Bongo lakini kwa Mimi Mars anaweza akawa ndio msanii wa kwanza kutamani kufanya naye,” amesema Galaxy.

Msanii huyo ameongeza kuwa muda wowote ataachia remix ya wimbo wake ‘Top In My Heart’ aliomshirikisha msanii wa Nigeria.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents