Michezo
Gareth Bale aifungia Wales goli muhimu katika michuano ya Ulaya
Timu ya taifa ya Wales huenda ikawa imechungulia kufuzu kucheza michuano ya mataifa ya Ulaya baada ya kushindwa kufuzu kwa takribani miaka 57 iliyopita.
Hii ni baada ya kupata ushindi wa dakika za lala salama wa goli 1-0 wakati ikicheza na Cyprus jana kwenye mechi ya kuwania kufuzu kucheza michuano ya Ulaya mwaka 2016.
Shujaa wa mechi hiyo alikuwa ni Gareth Bale aliyefunga goli hilo kipindi cha pili kwenye dakika ya 82 akiunganisha kwa kichwa krosi ya Jazz Richards na mpira kutinga moja kwa moja ndani ya nyavu za juu za Cyprus na kufungulia sherehe kwa mashabiki wa Wales waliosafiri kwenda Cyprus kuishangilia timu yao.
Hivi ndivyo msimamo ulivyo sasa