Michezo
Gary Cahill asaini mkataba mpya Chelsea
Mchezaji Gary Cahill ambaye ni beki wa kati wa timu ya taifa ya England na klabu ya Chelsea amesaini mkataba mpya wa miaka minne na klabu yake.
Cahil alisajiliwa mwaka 2012 akitokea timu ya Bolton, kwa dau la pauni milioni 7.
Mkataba wa sasa wa beki huyo kisiki ulikua umalizike mwishoni mwa msimu huu wa ligi, baada ya kusaini mkataba mpya Cahill alisema, “nimefanikiwa zaidi nikiwa hapa nitaendelea kujifunza, na kuisaidia timu yangu katika kutwaa mataji katika miaka minne ijayo.”
Katika msimu huu Cahil amecheza michezo 10 ya ligi kuu nchi England