Genge na Bongo Fleva kuleta raha jumamosi
KUNDI la muziki la Ukoo Fulani toka Kenya, wameshuka ndani ya Tanzania kwaajili ya kutoa burudani mchanganyiko wa muziki wa Genge toka Kenya na Bongo Fleva ya Tanzania, kwa pamoja katika uzinduzi wa albamu ya Vunja Winga ya mwanamuziki wa kundi hilo Sharama. katika kundi hilo wamefika wasanii watatu akiwa na Rich Rich na Abbass, huku wakisindikizwa na wasanii kibao toka Tanzania.
Katika uzinduzi huo unaofanyika siku ya juma mosi pale Daimond, pia kutakuwa na uzinduzi wa msanii mwingine toka kundi la Akudo Impact anayejulikana kama Totoo ze Bingwa.
wasanii wengine ni Twenty Percent, Zola D, Benjamin wa Mambo Jambo, Akudo Impact na wengine wengi.
Sharama akiwa kwenye pozi
Rich Rich kutoka Ukoo Fulani Kenya
mwanamuziki Abbas kutoka Kenya
{hwdvideoshare}id=1535|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}
Sharama akieleza jinsi shoo hiyo itakavyokuwa.
{hwdvideoshare}id=1536|width=400|height=300|tpl=playeronly{/hwdvideoshare}
Mwanamuziki Rich Rich, akitoa mistari jinsi atakavyo pagawisha