Gerrard amkingia Kifua Capello
Naodha wa Liverpool Steven Gerrard amesema hakuna kocha mwenye historia nzuri ya kuinoa England vema kama Fabio Kapello.
Mchezaji huyo amesema Kapello ana uwezo mkubwa na bila shaka kikosi kitapata mafaniko katika michuano ya kimataifa ya Ulaya Euro 2010.
‘Kitu cha maana nikuona kocha wetu ameendelea kuaminiwa licha ya kufanya vibaya katika michuano ya kombe la Dunia,’alisema Gerrard
‘Hivi ni nani mwenye uwezo mkubwa na mafanikio ya kuridhisha kama Fabio Kapello ?’ alihoji.
Ni jambo la kipuuzi la kumfukuza kocha kwasababu hakupata mafanikio kwenye mchuano mmoja (fainali za kombe la dunia), huku tukitafuta mwingine na kutegemea atafanya vizuri katika kipindi kifupi.
Kila mtu anafahamu mchezo wa soka niwa ajabu na mambo mabaya yanapotokea lawama zote hutua kwa kocha.’