BurudaniHabari

Gidi Gidi Maji maji ndani ya Marekani

Gidi Gidi  Kundi la muziki la Gidi Gidi Maji Maji lenye maskani yake nchini Kenya na kufanyia shughuli zake za kimuziki kule Cape Town, Afrika Kusini litakuwa ni kundi la kwanza kutoka ukanda wa Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye tamasha kubwa la Reggae linalokwenda kwa jina la Reggae on the River Festival.


 

Gidi Gidi

 

 

Story by: Daniel Nyalusi

Kundi la muziki la Gidi Gidi Maji Maji lenye maskani yake nchini Kenya na kufanyia shughuli zake za kimuziki kule Cape Town, Afrika Kusini litakuwa ni kundi la kwanza kutoka ukanda wa Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye tamasha kubwa la Reggae linalokwenda kwa jina la Reggae on the River Festival.

Tamasha hilo litafanyika mwezi ujao nchini Marekani kwenye Jimbo la California ambalo litahudhuriwa na wasanii wakubwa kwenye Muziki wa Reggae, Ragga na Dancehall.

Wakiongea kwa simu kutoka Afrika Kusini wasanii hao wamesema wamepata nafasi ya kuperform na kuonesha uwezo wao mbele ya wasanii wakubwa kama Sean Paul, Sizzla, Israel Vibration, Ziggy Marley, Anthony B na wengine kibao kutoka Jamaica na Ulaya.

Msemaji wa kampuni inayoandaa Judy Mowatt alisema Gidi Gidi Maji Maji hawatakuwa peke yao kutoka Afrika bali watashirikiana na Knaan msanii wa kisomali anayetamba katika Muziki huko majuu na anayefanya shughuli zake za kisanii nchini Canada na Salif Keita kutoka nchini Mali.

Source: Bongo5

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents