Burudani
Gigy Money adai Prezzo ni chawa
Video vixer na msanii wa Bongo Flava Gigy Money amedai kuwa rapper kutoka 254 Kenya, CMB Prezzo ndiyo aliyeanza kumfuata shoga yake Amber Lulu Bongo.
Gigy ametoa maneno hayo kupitia E-Newz ya EATV na kudai kuwa rapper huyo ni chawa na ndiyo aliyeanza kushoboka kwa rafiki yake na kuamua kutinga Bongo.
“Prezzo chawa tu kama chawa wengine tunaweka, we kamshobokea katoka Kenya kuja Bongo unashangaa nini, umemuona Lulu ameenda Kenya mzuri huyo sio mbaya kwa hiyo nyiye tulieni tu na wengine watakuja kutoka Mardagasca, UK,” amesema Gigy Money.
Siku chache zilziopita rapper Prezzo alitinga Bongo na picha zikaonyesha yupo na Amber Lulu, huku tetesi zikidai kuwa wawili hao wapo katika mahusiano ya kimapenzi.