Burudani

Gigy Money adai Prezzo ni chawa

Video vixer na msanii wa Bongo Flava  Gigy Money amedai kuwa rapper kutoka 254 Kenya, CMB Prezzo ndiyo aliyeanza kumfuata shoga yake Amber Lulu Bongo.

Gigy ametoa maneno hayo kupitia E-Newz ya EATV  na kudai kuwa rapper huyo  ni chawa na ndiyo aliyeanza kushoboka kwa rafiki yake na kuamua kutinga Bongo.

“Prezzo chawa tu kama chawa wengine tunaweka, we kamshobokea katoka Kenya kuja Bongo unashangaa nini, umemuona Lulu ameenda Kenya mzuri huyo sio mbaya kwa hiyo nyiye tulieni tu na wengine watakuja kutoka Mardagasca, UK,” amesema Gigy Money.

Siku chache zilziopita rapper Prezzo alitinga Bongo na picha zikaonyesha yupo na Amber Lulu, huku tetesi zikidai kuwa wawili hao wapo katika mahusiano ya kimapenzi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents