Giroud adai Mungu amehitaji abaki Chelsea
Olivier Giroud anaamini Mungu amemuhitaji yeye aendelee kubaki Chelsea baada ya striker huyo kuongeza kandarasi ya kusalia the Blues.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 watu wengi walitarajia angeondoka Stamford Bridge mwezi Januari ili kupata nafasi ya kucheza zaidi itakayomsaidia kuendelea kuitumikia timu yake ya taifa inayonolewa na Didier Deschamps katika michuano ya Euro 2020.
Lakini, Giroud aliwashangaza wengi baada ya kutokea benchi kwwenye mchezo wa Premier League dhidi ya Manchester United.
Giroud kisha akaja kuanza kwenye michezo mitano iliyofuata ya Frank Lampard huku akifunga goli kwenye ushindi wa mechi ya nyumbani dhidi ya Tottenham na Everton kabla ya Premier League kusimamishwa kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona.
Na kupelekea, Giroud kuongezewa mkataba ambao utamfanya kuendelea kusalia Stamford Bridge hadi mwisho wa msimu ujao.
”Nilipaswa kuondoka dirisha la mwezi Januari, kwa sababu sikucheza vyakutosha nilihitaji michezo zaidi ili kuwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa kwenye michuano ya Euro 2020,” amesema Giroud.
”Ilikuwa bado kidogo tu mimi kuondoka ndani ya klabu lakini hakika nafikiri Mungu alihitaji mimi niendelee kuwa hapa Chelsea. Kocha aliniambia kuwa asingeliweza kuniacha niondoke kwasababu hakuwa na mtu yoyote wa kuchukua nafasi yangu.