Burudani
Godzilla aeleza kwanini video ya ‘Stay’ imechelewa kutoka
Godzilla amesema ameshindwa kufanya maandalizi ya video ya wimbo wake ‘Stay’ kutokana na watu wengi kuwa busy na masuala ya uchaguzi.
Godzilla ameiambia Bongo5 kuwa mashabiki wengi wa muziki wameelekeza macho na masikio yao kwenye matokeo ya uchaguzi na hivyo kutokuwa na muda wa kufuatilia muziki kwa ukaribu.
“Sasa hivi hata ukiupdate kitu unakuta respond ndogo,” amesema. “Nikaona ngoja nisubiri kwanza uchaguzi upite halafu ndio nianze masuala ya ku-shoot video. Kwa sababu watu wako busy sana na masuala ya matokeo ya uchaguzi, sasa hivi ukifanya kazi yako unahitaji watu wawe attention na kitu chako,” ameongeza.