Habari
Goethe Institute kuwakaribisha Naledi
Katika kuwaunga mkono wabunifu vijana nchini Tanzania, taasisi isiyo ya kiserikali Goethe Institute itaikaribisha nyumba ya mitindo Naledi Fashion house pamoja na mtandao wa wabunifu Tanzania katika hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya shule ya kwanza ya ubunifu.
Mnada huo utahusisha nguo za wabunifu tofauti tofauti wa kitanzania ambazo zitaonyeshwa na walimbwende wa kitanzania ambao wamewahi kushinda mataji ya Miss Tanzania.
Vitu vingine vitakavyonadiwa ni pamoja na picha mbalimbali vinyago vya kuchonga na michoro ya wanasanaa wa fani hiyo. Burudani katika onyesho hilo italetwa kwenu na Karola Kinasha pamoja na bendi ya Ashimba.