Michezo
Golden State Warriors yachukua ubingwa wa NBA
Timu ya kikapu ya Golden State Warriors imechukua ubingwa wa ligi kuu ya mchezo huo ya Marekani, NBA.
Huo ni ushindi wa kwanza wa timu hiyo tangu mwaka 1975, miaka 40 iliyopita.
Warriors wamewafunga Cleveland Cavaliers pointi 105-97 kwenye mchezo wa sita wa fainali za NBA iliyomalizika alfajiri ya Jumatano hii kwa majira ya Afrika Mashariki.
Stephen Curry na Andre Iguodala walifunga pointi 25 kila mmoja.
Curry aliyewahi kuja Tanzania mwaka 2013 ndiye aliyekuwa nyota wa michezo yote sita ya kuwania fainali ya ligi hiyo.