Michezo

Golden State Warriors yachukua ubingwa wa NBA

Timu ya kikapu ya Golden State Warriors imechukua ubingwa wa ligi kuu ya mchezo huo ya Marekani, NBA.

11355115_738041372973765_164465367_n

Huo ni ushindi wa kwanza wa timu hiyo tangu mwaka 1975, miaka 40 iliyopita.

Warriors wamewafunga Cleveland Cavaliers pointi 105-97 kwenye mchezo wa sita wa fainali za NBA iliyomalizika alfajiri ya Jumatano hii kwa majira ya Afrika Mashariki.

Stephen Curry na Andre Iguodala walifunga pointi 25 kila mmoja.

Curry aliyewahi kuja Tanzania mwaka 2013 ndiye aliyekuwa nyota wa michezo yote sita ya kuwania fainali ya ligi hiyo.

steph-nets-2

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents