Michezo

Golden State Warriors yaipa somo Cavaliers NBA

Majira ya alfajiri ya kuamkia leo siku ya Jumanne huko nchini Marekani katika ligi ya mpira wa kikapu ya NBA kulikuwa na mchezo mkubwa ambapo timu ya Golden State Warriors ilipo cheza na Cleveland Cavaliers na kufanikiwa kuchomoza na ushindi wa jumla ya vikapu 118-108.

Silaha kubwa ya Warriors dhidi ya Cavaliers ilikuwa ni wachezaji wake Kevin Durant ambaye amefunga vikapu 32 na Stephen Curry aliyetupia 23 na kuiyongoza timu hiyo kuchomoza na ushindi huo.

Katika mchezo huo uliyokuwa wakuvutia kila timu ilionyesha ufundi na wachezaji wakiwa wenye ujuzi wa hali ya juu kiasi kwamba kivutia wapenzi wa mchezo huo waliyohudhuria katika Uwanja huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents