Michezo
Golikipa wa Marekani Tim Howard avunja rekodi ya kombe la dunia kwa kuokoa mipira mingi ya golini
Golikipa wa Marekani, Tim Howard jana amevunja rekodi ya dunia kwa kuokoa mipira 15 ya hatari golini kwakuwa kitu kama hicho kilifanyika kwa mara ya kwanza 1966.
Mlinda mlango wa Peru, Ramon Quiroga alikuwa anashikilia rekodi nyingine kwa kuokoa mipira 13 wakati timu yake ikicheza na Uholanzi mwaka 1978. Pamoja na jitihada hizo, Marekani ilitolewa na Ubelgiji kwa kufungwa mabao 2-1. Kutokana na hatua hiyo, Howard amegeuka kuwa shujaa wa Marekani na jina lake limetrend kwenye Twitter.