Burudani
H_art The Band na Lady Jaydee kuachia wimbo wao Ijumaa hii
H_art The Band kutoka Kenya na Lady Jaydee wameshirikiana katika wimbo wao wa pamoja ‘Rosella’ ambao unatarajiwa kutoka Ijumaa hii.
Kutokana na maneno ya Jaydee katika mtandao wa Instagram, wimbo huo utatoka pamoja na video yake siku hiyo hiyo.
“Subscribe sasa kwenye YouTube channel ya Lady JayDee Ili itakapofika Ijumaa paaaap Uwe wa kwanza kuona video ya Rosella ????????+ ???????? @h_arttheband & @jidejaydee,” ameandika Jide katika mtandao huo. Hata hivyo March 31 hitmaker huyo wa ‘Sawa na Wao’ anatarajia kuachia albamu yake ya saba ‘Woman’.