Michezo
Habari nzuri kwa mashabiki wa Arsenal, Bellerin athibitisha kuanza kupona majeraha yake
Katika mchezo uliofanyika mapema mwezi januari ambapo tulishuhudia Arsenal wakiitandika Chelsea bila huruma kwa jumla ya goli 2-0 katika dimba la Emirates, ulipelekea beki wa Arsenal Hector Bellerin kupata majeraha ya goti.
Baada ya kupata majeraha hayo na kupelekea kufanyiwa opereshini ya goti, beki huyo raia wa Uhispania amepost picha ikimuonyesha akiwa Hospitalini akimpigia daktari na kumuuliza “Docta naweza kutoka nje ya Hospitalini sasa?”
By Ally Juma.