Habari

Hakuna kitu kinaitwa UKAWA – Humphrey Polepole

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema kuwa hakuna kitu kinaitwa UKAWA kwani mpango huo ulianzishwa na CHADEMA ili kuvitumia vyama vingine kisiasa.

Humphrey Polepole

Polepole amesema kuwa kama UKAWA ingelikuwepo hadi leo basi isingetokea baadhi ya majimbo CHADEMA kushindana na CUF ile hali vyama vyote vipo chini ya muavuli wa UKAWA.

“Hakuna kitu kinaitwa UKAWA, hii ilikuwa project ya Chadema ikivitumia vyama vingine, CUF, NCCR na NLD. Kilichobaki ni UKIWA, katika jimbo lililokuwa la CUF leo CDM na CUF wanamenyana,”ameandika Humphrey Polepole kupitia Twitter.

Hata hivyo, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni CUF kwa upande wa Prof Lipumba imesimamisha mgombea wake huku CHADEMA nao wakisimamisha mgombea wao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents