Michezo
Hamilton ashinda mbio za ‘Russian Grand Prix’
Dereva wa Mercedes, Lewis Hamilton ameibuka mshindi wa mbio za Russian Grand Prix.
Huo ni unakuwa ushindi wa tatu wa dunia.
Hamilton alikuwa katika nafasi ya pili kuelekea dakika za mwisho mwisho za mashindano hayo kabla ya dereva mwenza wa Mercedes Nico Rosberg kukabiliwa na matatizo ya injini.
Mjerumani Nico Rosberg alilazimika kuyaaga mashindano aliposhindwa kupata kasi. Hamilton ameshinda hadi sasa mashindano 9 msimu huu na hivyo anahitaji alama 9 pekee kutawazwa bingwa mara tatu wa duniani.