Burudani

Harmorapa achafua hali ya hewa, ‘Master J mbona simjui’

Ni kweli nilichokisikia au ninaota? Eti Harmorapa hamfahamu Master J?

Rapper huyo ameonekana kuwashangaza mashabiki Jumatano hii wakati alipokuwa katika kipindi cha Kikaangoni cha EATV kuwa hamfahamu mtayarishaji huyo mkongwe wa muziki nchini.

“Master J mbona simjui? Sidhani kama ni producer maana hakuna ngoma yake yoyote inayohit ambayo mimi naijua,” amesema Harmo.

Hitmaker huyo wa ‘Kiboko ya Mabishoo’ ameongeza kwa kusema kwamba ataachia wimbo wake mpya mwezi ujao ambao umetayarishwa na P-Funk huku video yake ikiongozwa na Karabani.

Kauli hiyo ya kejeli ya Harmorapa kwa Master J, imekuja baada ya hivi karibuni producer huyo wa muziki kudai kuwa Hamorapa siyo msanii direct bali ni mburudishaji kama wasanii wengine waliowahi kupita akiwemo marehemu John Walker.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents