Habari

Hatimaye Odinga ajiapisha kuwa Rais wa Kenya mbele ya maelfu ya watu

Lile Zoezi kubwa na la kihistoria nchini Kenya la kuapishwa kwa Kiongozi wa upinzani nchini humo, Raila Odinga limekamilika ambapo maelfu ya watu wamehudhuria tukio hilo katika viwanja vya Uhuru Park jijini Nairobi.

Raila Odinga akiapa

Odinga amesema atawatumikia Wakenya na kutimiza ahadi zake zote alizowapa kipindi cha uchaguzi mkuu wa Urais mwaka jana.

Hata hivyo, wakati Odinga akiapa mbele ya umati huo Mgombea mwenza Kalonzo Msyoka na viongozi wa juu wa NASA kama Musalia Mudavadi hawakuhudhuria kwenye sherehe hizo.

Tazama baadhi ya picha hapa chini za tukio hilo;

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents