Habari
Hatimaye Rais Robert Mugabe amejiuzulu
Spika wa bung la Zimbabwe ametangaza rasmi kuwa Rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe amejiuzulu nafasi ya urais aliyoishikilia kwa miaka 37.
Kumekuwa na shangwe miongoni mwa wabunge kufuatia tangazo hilo lililotolewa muda mfupi uliopita huku mchakato wa kumuondoa madarakani rais huyo kupitia Bunge ukiwa umesitishwa.
Kupitia ukurasa wa rasmi wa Twitter wa Chama tawala nchini humo cha Zanu-PF kimethibitisha taarifa hizo kwa kuandika “R G Mugabe amejiuzulu. Safari ya zama mpya inaanza rasmi”
R G Mugabe has resigned. The New Era has begun!
— ZANU PF (@zanu_pf) November 21, 2017