Habari

Hawa wa Diamond kufanyiwa upasuaji leo India, akutwa na ugonjwa mwingine sio Ini kama ilivyoelezwa Bongo

Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale ametoa taarifa kuwa msanii wa muziki nchini Hawa Said maarufu kama Hawa wa Diamond atafanyiwa upasuaji wa moyo jioni ya leo nchini India.

Babu Tale

Babu Tale ambaye aliondoka nchini na Hawa wiki iliyopita kwenda India kwa ajili ya matibabu, amesema kuwa Wataalamu wameangalia kila kitu na hawajaona tatizo kwenye Ini kama iliyokuwa inaripotiwa awali.

Asante Mungu tumefika salama India na tumefanya vipimo vyote upya salama na jibu lililotoka kwa wataalamu kwa asilimia 95% awajaona tatizo linalohusiana na ini kwa mgonjwa ila ni moyo ndio uliokua unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini ivyo basi kutaitajika kufanyika upasuaji mkubwa ambao utakua na uangalizi mkubwa wa wataamu then wametuakikishia baada ya hapo mgonjwa atapata nafuu na inawezekana izo 5% zilizobaki itakua poa na tatizo la ini alitokuwepo kikubwa tunaomba mtuombee dua na msiache kumuombea pia @diamondplatnumz apatenguvu ya kuendela kumsaidia kwa maana kutoa ni moyo. Kikubwa sana naomba tumuombee Hawa coz anaingia kwenye upasuaji mkubwa na hii ni atua ya yeye kua salama. Mungu tusimamie

Kwenye matibabu hayo nchini India, Diamond Platnumz amelipia gharama zote, ili kumsaidia msanii mwenzake ambaye miaka ya nyuma walishawahi kufanya naye kolabo ya wimbo wa Nitarejea.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents