Michezo
Haya ndio maamuzi ya Steven Gerrard katika soka
Mchezaji wa zamani na nahodha wa Liverpool Steven Gerrard ametangaza rasmi kustaafu kucheza soka baada ya kuachana na klabu ya LA Galaxy ya MLS.
Gerrard mwenye umri wa miaka 36, ameamua kutundika daluga baada ya kuwepo katika mchezo huo wa soka kwa miaka 19 akicheza vilabu vya Liverpool , LA Galaxy pamoja na timu ya Taifa ya England.