Michezo
Haya ndo majibu ya kocha wa Simba Mayanja kuhusu mchezaji Said Ndemla
Kocha wa Simba Jackson Mayanja amejibu swali la waaandishi wa habari juu ya kiungo wa Simba ambaye pia anayeichezea timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Said Hamisi Ndemla kwanini hampi nafasi kwenye kikosi cha Simba toka kocha Mayanja aanze kazi.
Wataalamu wa mambo ya soka wanasema Ndemla ameichezea Simba sio zaidi ya dakika 50 hadi sasa. Haya ndo majibu ya kocha Jackson Mayanja.
“Kwanza inabidi watu wajue mchezo wa soko siyo timu ya taifa namie siifundi Simba kwajili ya timu ya taifa siyo lazima mchezaji akichezea timu ya taifa na Simba acheze mimi naifundisha Simba kwa kile ninacho kiamini pamoja na mipango yangu Ndemla ni mchezaji mzuri sana na bado na mtaarisha na mtamwona siyo mda na atarudi kwa vile jinsi nataka awe vizuri zaidi”