Michezo

Hiddink akiri kuwa mambo ni magumu kwa Chelsea

Kocha wa muda wa timu ya Chelsea, Guus Hiddink amekiri kuwa ni ngumu kwa timu yake kuingia kwenye nne bora ya ligi nchini Uingereza msimu huu.

guus-hiddink-chelsea-premier-league-20160301_6qx87f4cxm5s1qo2wrj5jcwor

Baada ya kutoka Chelsea kutoka sare kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Stamford Bridge kwa kufungana goli moja kwa moja na timu ya Stock City, Guus Hiddink amesema ni ngumu kwa Chelsea kuingia kwenye nne bora msimu huu ambayo itaiwezesha timu hiyo kucheza michuano ya ligi ya mabingwa ulaya (Uefa) msimu ujayo.

“Nne bora haiwezekani tena, tulinusurika kuingia kwenye hatari ya kushuka daraja mwezi Desemba, na tumejiweka salama ndani ya muda mfupi sana,” alisema Hiddink.

“Kupanda katikati ya msimamo wa ligi, kwa kiwango cha kawaida cha Chelsea, haitoshi,” aliongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents