Michezo

Higuain atundika daluga Argentina

Mshambuliaji wa Chelsea, Gonzalo Higuain ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa lake la Argentina.

Higuain, 31, ameshiriki kwenye michezo 75 ya timu ya taifa na kufunga mabao 31, lakini hajaitwa tena kwenye timu hiyo tangu kumalizika kwa michuano ya kombe la dunia 2018.

“nimefanya maamuzi kwasababu nataka nifurahie familia yangu, nataka nitumie muda mwingi na binti yangu wakati huo huo nahisi nimeipa nchi yangu kile nilichoweza ‘’ amesema Higuain

Aidha, Higuain amesema anataka kuelekeza nguvu kuitumikia klabu yake ya Chelsea aliyojiunga nayo kwa mkopo mwezi Januari akitokea Juventus.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents