Michezo
Hii hapa droo ya kombe la FA
Droo ya raundi ya nne ya kombe la FA imetoka huku timu za ligi kuu ya England zikipangwa na zile za daraja la chini.
Arsenal, ambao ndio mabingwa watetezi wao wamepangwa kucheza na timu ya Burnley, huku Chelsea wao wataanzia ugenini kwa kucheza na mshindi wa mchezo kati ya Northampton Town au Mk Dons.
Man City wao watakipiga na mshindi wa mchezo wa Wycombe Wanderers au Aston Villa. Man United wao watakipiga na Derby County.
West Ham, wanasubiri mshindi wa mchezo unaowakutanisha Exeter City dhidi ya majogoo wa Anfield Liverpool. Michezo hii ya raundi ya nne itachezwa January 29 mpaka Februari 1