Michezo
Hii ndio droo ya 16 bora UEFA Champions League, Arsenal uso kwa uso na Barcelona
Hii ndio ratiba ya mechi za raundi ya 16 bora katika ligi ya mabingwa barani Ulaya (UEFA champions League) iliyopatikana baada ya droo iliyokuwa ikichezeshwa kukamilika.
Droo hiyo ilifanyika mjini Nyon, Uswisi. Hii itakuwa mara ya tatu kwa Chelsea kukutana na PSG katika michuano ya UEFA.
Arsenal ya Uingereza imepangwa na Barcelona ya Uhispania, ambao ndio mabingwa watetezi.
Mechi hiyo itakuwa kama marudio ya fainali ya 2006, ambayo mabingwa hao wa Uhispania walishinda 2-1 kupitia mabao mawili ya dakika za mwisho mjini Paris.