Michezo

Hii ndio michezo atakayeikosa beki wa Manchester United Luke Shaw baada ya kupata majeraha

Hii ndio michezo atakayeikosa beki wa Manchester United Luke Shaw baada ya kupata majeraha

Beki wa kushoto wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya England Luke Shaw aliyepata mshtuko baada ya mgongano wa bahati mbaya na beki wa Uhispania Dani Carvajal katika nusu ya pili ya mchezo uliowakutanisha miamba hao wawili ambapo England akiwa nyumbani alifungwa goli 2-1 na Hispania

Baada ya majeraha hayo ya kichwa Shaw alirudi United kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi na matibabu siku ya Jumatatu licha ya beki huyo kuumia wakati anaitumikia timu yake ya taifa.

akiongea na wanahabari kocha wa timu ya taifa ya England Gareth Southgate alisema ” Hakuna mtu aliyetamani kuona tukio kama hilo”na kuongeza kuwa Shaw alitolewa uwanjani akiwa amefungwa vifaa vya kumuingizia hewa ya oksijeni lakini alisema kuwa amepata tena ufahamu haraka katika chumba cha matibabu, na hivi karibuni alikuwa akiwasiliana na marafiki na familia.

Baada ya beki huyo kisiki mwenye ustadi wa aina yake kuumia katika mchezo huo wa jumamosi dhidi ya Uhispani huku kocha wake Jose Mourinho akishuhudia jukwaani, msaada wa beki huyo utakosekana katika timu yake ya Manchester United katika mchezo wao wa siku ya jumamosi dhidi ya Watford,hivyo Luke Shaw hatakuwepo kwenye mchezo huo utakaofanyika katika dimba linalomilikiwa na The Golden Boys au jeshi la njano Watford linalojulikana kama Vicarage Road Stadium.

Siku chache kabla, Shaw alikuwa amefungua hadithi ya hofu ya mguu wake uliovunjika, ambalo alikiri alikuwa karibu na kumchukuliwa na kumlazimisha kufikiria kustaafu kutoka mchezo huo kwa umri wa miaka 23 tu.

 

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents