Hii ndio ngoma iliyomtangaza zaidi Joh Makini kimataifa
Mkali wa muziki wa Hip Hop kutoka kundi la Weusi, Joh Makini amesema kolabo yake na AKA ‘Don’t Bother’ imemtangaza zaidi kimataifa na kumpa heshima.
Joh makini amesema kolabo hiyo imemuongezea thamani na imemtambulisha nje kwa kiwango kikubwa sana, mpaka anapata air time kwenye nchi kama South Africa na watu wanamjua kwa kiwango fulani, ni kwa sababu ya kolabo hiyo.
“Ukitaja wasanii ambao wapo mainstream pale South Africa huwezi kuacha kumtaja AKA, kiasi kwamba hata wasanii wa pale kumpata kwa kolabo inakuwa ni ngumu,” Joh Makini ameimbia Clouds Fm na kuongeza.
“Kufanya kazi na mtu kama yule kwanza inakutengenezea Respect alafu inaonyesha userious ulionao na watu lazima waheshimu hilo, unapofanya kazi wasikuchukulie poa. Hatujawahi kuongea kwamba tutoe ngoma yake au yangu pengine siku za mbeleni,” amesema Joh Makini.
By Peter Akaro