Michezo

Hii ndio ratiba ya nusu fainali ya kombe la UEFA na Europa League

Hatimaye droo ya hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la UEFA na ligi ya Europa imepangwa Ijumaa hii.

Katika kombe la UEFA, mahasimu wa mji wa Madrid ambao ni Real madrid na Athletico Madrid wamepangiwa kukutana katika hatua hiyo huku nusu fainali ya pili ya kombe hilo likiwakutanisha Monaco dhidi ya Juventus. Mechi hizo zinartarajia kuchezwa Mei 2 na 3 huku mechi za marudiano zikitarajiwa kufanyiaka Mei 9 na 10.

Wakati huo huo katika Europa League Manchester United imepangwa kukutana na Celta de Vigo ya Hispania,nao Ajax watachuana dhidi ya Olympique Lyon.

Michezo hiyo inatarajiwa kuchezwa Mei 3 na 4 kwa michezo ya kwanza huku mechi za marudiano zikitarajiwa kurudiwa Alhamisi ya Mei 11.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents