Burudani

Hii ndio sababu ya show ya Drake ya Amsterdam kuvunjika

Drake alilazimika kuivunja show yake ya mjini Amsterdam Jumatatu hii baada ya kudaiwa kuugua ghafla. Kumbe rapper huyo alikula chakula chenye sumu!

Mtu wa karibu wa rapper huyo ameuambia mtandao wa TMZ kuwa rapper huyo alikula chakula hicho chenye sumu muda mfupi kabla ya kufanyika kwa show hiyo.

Drake alikimbizwa hospitali ndipo madaktari walipomshahauri kutofanya show hiyo. Mashabiki walimsubiri rapper huyo katika ukumbi wa Ziggo Dome kwaajili ya kutumbuiza kwa muda wa dakika 75 kabla ya kutangaziwa kuvunjika kwa show hiyo.

Hata hivyo show hiyo inatarajiwa kufanyika tena Jumatano hii katka ukumbi huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents