Hii ndiyo siri ya Paul Pogba kutupia mabao dhidi ya Huddersfield
Kiungo wa Manchester United, Paul Pogba alikuwa kwenye wakati mzuri usikuwa jana baada ya mpenzi wake, Maria Salauses alipohudhuria mechi yao dhidi ya Huddersfield ambapo nyota huyo alifanikiwa kufunga jumla ya mabao mawili kwenye ushindi wa magoli 3-1 ikiwa ni siku ya Boxing.
Pogba akitoka kwenye misukosuko ya kutoelewana na aliyekuwa meneja wa timu hiyo, Jose Mourinho lakini Mfaransa huyo kwa sasa anaonekana akiwa na furaha akiwa chini ya Ole Gunnar Solskjaer.
Siku chache zijazo Pogba anatarajiwa kuitwa baba kutokana na mpenzi wake Maria Salaues raia wa Bolivia mwenyeumri wa miaka 23 kuwa na ujauzito.
Salaues alikuwa kwenye dimba la Old Trafford usiku wa Jumatano bila kujali hali yake ya ujauzito alikwenda kumuunga mkono Pogba.
United imeshinda michezo yake yote ikiwa chini ya meneja, Solskjaer huku kiungo huyo akiwa na mchango mkubwa kwenye matokeo hayo.
Manchester United sasa inajiandaa kuwakabili Bournemouth Jumamosi hii kwenye uwanja wa nyumbani huku wakihitaji ushindi ili kutengeneza mazingira mazuri zaidi kwenye msimamo wa Premier League.