Michezo
Hii ndio sababu iliyomfanya Ryan Giggs kutokuwepo uwanjani, Man Utd vs Stoke
Ryan Giggs jana hakuwepo kushuhudia mchezo ambao timu yake ilipata ushindi wa bao 3-0 dhidi ya Stoke City katika uwanja wa Manchester United, Old Trafford kutokana na matatizo ya kifamilia, ililipotiwa na gazeti la Daily Mail kutoka England.
Kocha Louis Van Gaal alionekana kutumia muda mwingi wa mechi hiyo kushauriana na makocha wengine wa mazoezi huku kiti cha msaidizi wake Ryan Giggs kikibakia wazi.
Kiti ambacho huwa anakalia Ryan Giggs kikiwa cheupe
United ilipata magoli yaliyofungwa na Jesse Lingard, Anthony Martial na nahodha Wayne Rooney yaliweza kumpa pumzi kocha Louis Van Gaal ambaye kwa sasa anapitia kipindi kigumu akiwa Old Trafford.