Michezo
Hiki ndicho atakachokifanya Toure baada ya wiki moja aliyowapa Manchester City kumalizika
Mkataba wa Yaya Toure na timu yake ya Manchester City umebakiza mwaka mmoja kabla ya kumalizika.
Wakala wa Toure amesema wiki ijayo itafahamika hatma yake.
“Wiki ijayo tutajua kama Toure atasaini mkataba mpya au ataenda timu nyingine. Lakini kama ataondoka City hataenda timu nyingine ya Uingereza,” alisema Seluk.
aliongeza pia, “Kuna watu wanasema amekuja City kwaajili ya hela tu. Lakini alipokuja hapa timu ilikuwa inashika nafasi ya sita au saba na ilikuwa haijawahi kushiriki mashindano ya klabu bingwa Ulaya.”
Toure amebakiza mwaka mmoja mkataba wake uweze kuisha, pia ndio mchezaji anayeongoza kulipwa mshahara mkubwa wa paundi 220,000 kwa wiki.