Technology

Hiki ndicho kilichoifanya Disney isite kuinunua Twitter

Kampuni tajiri ya Walt Disney, ilisita kununua mtandao wa kijamii wa Twitter kutokana na kasumba ya unyanyasaji inayofanywa na watumiaji wake ambayo ingechafua heshima yake, kwa mujibu wa ripoti ya Bloomberg.

unnamed

Disney ilikuwa moja ya makampuni ambayo ilikuwa imetajwa kuwa kwenye mazungumzo ya kutaka kuununua mtandao huo unaotapatapa kifedha.

Tweets za matusi na kejeli zimekuwa maarufu kwenye mtandao huo. Mfano pindi Robin Williams amefariki, baadhi ya watumiaji wa Twitter walimshambulia binti yake hali iliyomfanya aifute app hiyo kwenye simu yake.

Mtandao huo umeshindwa kuhimili ukuaji wa mitandao mingine kama Facebook, Instagram na Snapchat.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents