Burudani
Hiki ndicho kilichowapeleka Shaa, AY, Chameleone na wengine Nairobi, wadaiwa kulipwa mkwanja mrefu!
Hivi karibuni wasanii mbalimbali wa Afrika Mashariki wakiwemo Shaa, AY, Jose Chameleone na Maurice Kirya waliungana na wenzao wa Kenya ambao ni pamoja na Nameless, Eric Wainaina na Rabbit walikutana jijini Nairobi Kenya kupika kitu kikubwa.
Wasanii hao walikuwa nchini humo kushoot reality TV show inayotarajiwa kuwa gumzo. Chanzo kimoja kimeliambia gazeti la The Star, kuwa ni show ya channel ya Maisha Magic.
Chanzo hicho kimesema gharama za utayarishaji wa show hiyo inaweza kufikia shilingi za Kenya milioni 100 hadi 200. Kilisema wasanii hao watakuwa wamelipwa ujira mnono.
Kama tulivyoandika awali, show hiyo inaweza kuwa ni ile ya kusaka vipaji iitwayo Maisha Superstar.