Hillary Clinton ashutumiwa kusababisha mauaji Libya
Mgombea wa Urais wa Marekani kupitia chama cha Democratic, Hillary Clinton ameshutumiwa kwa kusababisha mauaji ya vijana wawili nchini Libya yaliyotokea mwaka 2012.
Vijana hao waliokuwa wanafahamika kama Smith na Tyrone Wood wakati ubalozi wa Marekani uliposhambuliwa na majeshi ya Kiislam wakati wa vurugu za vita zilizofanyika wakati wa kumpindua aliyekuwa rais wa nchi hiyo marehemu Muammar Gaddafi.
Wazazi wa vijana hoa wamedai kuwa matumizi ya barua pepe binafsi zilichangia mauaji ya watoto wao.
Hata hivyo msemaji wa kampeni za Hillary Clinton amepinga tuhuma hizo zilizotolewa juu yake huku mgombea wa Republican, Donald Trump akizidi kuchafua kampeni za wapinzani wake kwa kuweka wazi mabaya aliyowahi kutenda Clinton alipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo.