Hitma ya Five Stars-part2
Wakina mama wakiwa kwenye maombelezi siku ya Hitma ya bendi ya muziki wa Taarab ya Five Stars, ambayo ilipata ajali wakitokea Morogoro kuja Dar es salaam mach 21, 2011 na kusababisha vifo vya watu 13 na majeruhi tisa.
Miongoni mwa Marehemu hao ni Issa Kijoti, Omari Tulu, Haji Babu, Sheba Juma, Omari Hasim, Tizo Mgunga, Hamisi Mipango, Husna Mapande, Samir Maulid, Hassan Ngereza, Rama Kinyoya, Nassoro Madege na …………
Huu nao ulikuwa upande wa Wanaume, nao walikuwepo kuwaombea dua marehemu.
Hapa mpenzi namba moja wa Five stars, akiwa pamoja na Meneja wa Tmk Wanaume Mkubwa fella (Fella aliyevaa kanzu kama nyeusi).
Teacher naye alikuwepo akiwasihi wasanii huu ni muda wa kuungana kwa pamoja, na wajifunze mshikamano kutokana na msiba huu.
Prince Hemed Mgeni, yeye ndiyo anakumbuka mengi kutoka kwa Issa Kijoti kwakuwa alikuwa naye katika bendi ya Zanzibar Star.
Mungu azilaze roho za marehemu, mahali pema peponi…………. Amin