Burudani
Hivi ndivyo Kanye West anavyomuumiza roho Jay Z (+Picha)
Msanii wa muziki wa Hip Hop, Kanye West amepost picha kwa mara ya kwanza akiwa na familia yake tangu aliposema anakwenda milimani kuandaa albamu yake Mwezi Mei.
Rapa huyo ambaye alionekana mara ya mwisho katika chakula cha usiku siku ya Wapendanao (Valentine Day) mwaka huu, amepost picha akiwa na familia yake pamoja na familia ya msanii aliyemsaini kwenye lebo yake ya GOOD Music, 2 Chainz.
Picha hiyo iliyopigwa siku ya Jana usiku nyumbani kwa Kanye West imeonekana ikizungumziwa zaidi baada ya msanii huyo kuamua kutaka kujitoa katika kampuni ya kuuza muziki ya Jay Z ya Tidal.
Na Laila Sued