Burudani

Hivi ndivyo mashabiki wa muziki Kenya wamjuavyo Nay Wa Mitego!

Leo Jumatano (June 12) mtangazaji maarufu wa Radio/TV Citizen ya Kenya Mzazi Willy M. Tuva, kupitia akaunti yake ya Facebook amewapa nafasi wasikilizaji wake kumuelezea wamjuavyo hit maker wa ‘Muziki Gani’ Nay Wa Mitego. Aliandika “Unajua nini kumhusu NEY WA MITEGO anayetamba na wimbo MUZIKI GANI featuring DIAMOND?

nay wa

Na haya ndio majibu ya mashabiki hao:

1. Cleigh Haruna: ni member wa illuminati
2. Bwana Sabasa: he is an hiphop artist
3. Allie Mvoi Mvoi Allie: Cmjui vizuri mlezi.
4. Kev Wilshere: Najua ni mjeuri very controvercial hip hop head wid mad talent.
5. Dennis Nyamboga: Mwenye aliwadis wasanii wa kitambo kama mr nice,dudu mbaya,misosi,sistr b.katika wimbo wake itafaamika tu
6. Wyza Laviguitar: namjua kama ambaye hupenda kuponda wasanii wenzake bila kujali
7. Prince Andy: Weuw.msee mwenye bif na wasee wanaotoboa pua kaka
8. Nay Lesious: Cmjui Vzr Tuambie Bac Mzazi
9. Antiba Bett Kemboi:Yeye ni msanii mwenye tatoo nyingi za ajabu sana.
10. Braden Feliciano: amenunua gari jipya na pia kanunua bastola

Nay amekuwa midomoni mwa watu kwa muda mrefu kutokana na aina ya uandishi anayotumia katika nyimbo zake kuwa ‘controversial’ na kuzua mijadala kila anapotoa wimbo mpya. Hit song yake aliyoshirikiana na Diamond Platnumz inazidi kumfungulia milango ya shows na kumfanya kuwa kati ya wasanii wenye show nyingi sana kwa sasa.

Jumapili iliyopita (June 8) katika tuzo za KTMA 2013 Nay alifanikiwa kuondoka na tuzo ya wimbo bora hip hop.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents