Hizi ndio klabu zenye vikosi ghali zaidi duniani, Utawashangaa Arsenal na Real Madrid
Wakati klabu nyingi duniani zikitumia mamilioni ya fedha kufanya usajili ili kuendana na ushindani wa mpira wa kisasa, hatimaye klabu za soka zenye vikosi vya ghali zaidi vimetangazwa.
Kwenye orodha hiyo ya timu 50 iliyotolewa na Taasisi ya CIES Football Observatory imeonesha kuwa timu kutoka Uingereza zimeongoza kwenye 10 bora.
Kwenye nafasi ya kwanza kwenye orodha hiyo Man City imeongoza ambapo kikosi chake kina gharama ya Euro milioni £777 ikifuatiwa na vikosi vya PSG Euro Milioni £713, Man United Euro milioni £661 na FC Barcelona Euro milioni £641 .
Katika hali ya kushangaza ni kwamba timu ambazo zinatajwa kuwa na mkwanja mrefu duniani za Real Madrid, Bayern Munich na Arsenal hazipo kwenye Tano bora ya klabu zenye vikosi ghali duniani licha ya kuingiza faida kubwa kwenye dili za matangazo, mikataba na makampuni na mauzo ya jezi.
Kwenye orodha ya vikosi ghali kwenye 10 bora Uingereza imetoa timu sita ikifuatiwa na Hispania timu mbili huku Italia na Ufaransa zikitoa timu moja moja.
Tazama orodha kamili ya timu 50 zenye vikosi ghali zaidi duniani kwa msimu huu 2017/18.