Habari
Hofu yazidi kutanda kuhusiana na afya ya Nelson Mandela
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela ametumia usiku wa pili akiwa mahututi kwenye hospitali usiku wa jana huku wanafamilia na watu wengine duniani wakihofia kuwa shujaa huyo wa Afrika anaweza kupoteza maisha muda wowote.
Gari chache zimeonekana leo asubuhi zikiingia kwenye hospitali hiyo ya Pretoria ambako Rais huyo wa zamani amelazwa.
Jana, Ras Jacob Zuma alisema kuwa “Rais wa zamani Mandela ameendelea kuwa mahututi hospitali.”