Hoteli zateketea Bagamoyo
Leo asubuhi hoteli mbili maarufu, Paradise Beach Resort na Oceanic Bay, ziliteketea kwa moto huko Bagamoyo.
Moto huo ulianza asubuhi na ulidumu kwa muda wa robo saa (dakika 15), kwa bahati nzuri hakuna mtu aliyejeruhiwa ila imeelezwa na wamiliki wa hoteli hizo kwamba jumla ya wafanyakazi 380 watakuwa hawana kazi baada ya janga hili.
Wasamaria wema walijitahidi kadiri ya uwezo wao kuuzima moto huo, lakini ilishindikana kuokoa kitu chochote na kusababisha hasara kubwa sana ya mamilioni.