Michezo
Howard Webb astaafu kupuliza kipenga
Refa maarufu England na Mataifa ya Ulaya, Howard Webb amestaafu kuchezesha soka baada ya kufanya kazi hiyo kwa miaka 25 na sasa atakuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa taasisi ya marefa (PGMOL).
Refa huyo mwenye heshima kubwa, amechezesha mechi zaidi ya 500 za Ligi Kuu ya England na nyingine za mashindano ya soka nchini humo tangu apande daraja mwaka 2003.
Webb pia amechezesha fainali mbili za Kombe la Dunia na mbili za Kombe la Mataifa ya Ulaya na kuweka rekodi ya kuwa refa wa kwanza kuchezesha fainali ya Euro na Kombe la Dunia kwa mwaka mmoja, 2010.
Webb alikuwa akishutumiwa sana kuibeba Manchester United.