Burudani
Huddah aweka mtandaoni kadi ya gari kuthibitisha kuwa ndiye mmiliki wa ile Range Rover
Mrembo wa Kenya, Huddah Monroe ameamua kuwakata vilimilimi wale waliokuwa wakimkebehi kuwa mkoko aina ya Range Rover anaotumia huenda sio wa kwake, kwa kuweka kithibitisho cha kadi ya gari hiyo ambayo imesajiliwa kwa jina lake halisi Sonie Alhuda Njoroge.
Mwaka jana mwishoni baada ya kushare picha za gari yake mpya, kuna baadhi ya blogs za Kenya zilizodai kuwa gari hiyo si yake.
Katika post hiyo ambayo ameifuta aliweka kadi hiyo na kuandika:
“I don’t like to prove anything to bastards but , I don’t rent or borrow cars! I hustle too hard to be living on a budget! Somebody tell these bloggers to go and get the final search at KRA , Bitches! #CozYouAreBrokeDontMeanEveryoneIs #PutSomeKYjellyOnYourLives”