Michezo
Huu ndiyo muonekano wa nywele za James Rodríguez
Football with a fashion. Mchezaji wa Real Madrid, James Rodríguez amewashangaza mashabiki baada ya kubadilisha muonekano wake wa nywele.
Baada ya hivi karibuni kumalizika kwa michuano ya kombe la Copa America, watu wameonekana wakimshangaa Rodríguez (24) kutokana na muonekano wake mpya wa nywele huko kwenye maeneo ya Miami Beach akiwa na mke wake Daniela Ospina pamoja na mwanae [Salome].
Huo ndiyo unaweza ukawa muonekano mpya wa Rodríguez kwenye msimu mpya wa ligi utakaoanza mwezi Agosti mwaka huu. Lakini pia Rodríguez anatajwa ni kama mmoja ya wenye muonekano mzuri zaidi wa fashion wakiongozwa na Cristiano Ronaldo pamoja na David Beckham.