Ibrahimovic kuendelea kubakia Manchester United
Klabu ya Manchester United imesema itamuongezea mkataba mpya wa mwaka mmoja mshambuliaji wake Zlatan Ibrahimovic kulingana maneno ya meneja Jose Mourinho.
Mchezaji huyo kutoka Sweden mwenye umri wa 35, alitua Old Trafford katika uhamisho wa bure katika msimu huu akiwa na uwezo wa kuongeza mkataba mwingine kwa msimu wa pili. Amesha funga mabao 17 katika mashindano yote msimu huu.
Mourinho alisema: Tutaanda mpango wa kuongeza mkataba wake kwa mwaka mwemgine .Baadaye anaweza kufanya atakacho.
Ibrahimoviv alisema: Najihisi vyema, nikiwa nitaendelea itakuwa mwaka mwengine.
Ibrahimovic ambaye ameshafunga mabao 62 katika mechi 116 akiichezea Sweden kabla ya kustaafu katika soka ya kimataifa mnamo mwezi Juni, alihama klabu ya PSG mwishoni mwa msimu uliopita