Habari

Ice Prince na Bonang kusherehesha tuzo za Channel O 2012

Zimebaki siku mbili tu hadi ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya tuzo za tisa za Channel O Music Video zitakazofanyika Jumamosi hii nchini Afrika Kusini.

Tuzo hizo zitamuonesha superstar wa Nigeria Ice Prince na Bonang wa Afrika Kusini wakiwa mamc wa tuzo hizo.

Bonang

Wawili hao wataendesha tuzo hizo zenye thamani huko Walter Sisulu Square, Kliptown, Soweto.

“I feel really honoured and super excited, I think I am more excited than anyone who has ever hosted/co-hosted the show because it’s a huge privilege to be hosting the biggest award show in Africa,” alisema Ice Prince.

“The Channel O Music Video Awards will be broadcast to over 40 African countries so you can only imagine how excited I am,” alisema Bonang.

Wasanii watakaopanda kwenye stage ni pamoja na kundi la Kenya la Camp Mulla, Khuli Chana (SA) M.anifest (Ghana), Pro, Mi Casa, DJ Zinhle na Bucie.

AY na Cpwaa wanaiwakilisha Tanzania.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents