Bongo Movie

Idris Sultan na Ernest Napoleon wapata shavu la kuonekana katika filamu ya Hollywood

Idris Sultan na muigizaji na mtayarishaji wa filamu za Kiumeni na Going Bongo, Ernest Napoleon wamepata nafasi ya kuigiza katika filamu mpya ya ‘The Blue Mauritius’ ya Marekani.

Filamu hiyo itaanza kutengenezwa mwezi Machi mwakani ambapo kazi hiyo inasimamiwa na kampuni mbili za utengenezaji wa filamu kutoka Marekani ikiwemo D Street Pictures na Benoraya Pictures.

Kwa mujibu wa barua ambayo imetolewa na kampui hizo, imeonyesha kuwa filamu hiyo itatumia kiasi cha dola milioni 17 ambapo ni sawa na shilingi bilioni 38 za kitanzania. Filamu hiyo itafanyika sehemu mbalimbali ikiwemo Cape town, Berlin, London, Paris, Acapulco, Mexico.


Picha za wasanii ambao watashiriki katika filamu ya ‘The Blue Mauritius’

Waigizaji wengine ambao watahusika katika filamu hiyo ni Pearl Thusi (Quantico), Eric Dane (The Last ship/Grey’s anatomy), Gerard Depardieu (Life of pie) John Rhys (Lord of the rings/Indiana Jones) Thomas Kretschmann (Avengers/Kingkong) na Derek de Lint (NCIS/Crossing Lines).

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents