Habari

In case umemiss: Kauli ya Sugu iliyosababisha bunge lisitishwe ghafla leo kuogopa uchochezi (audio)

Muda mfupi uliopita spika wa bunge, Anna Makinda amelazimika kusitisha shughuli za bunge mwanzoni tu mwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliyokuwa ikisomwa na waziri kivuli wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi aka Sugu.

waziri kivili wa whvum Joseph Mbilinyi akiwasilisha hptuba ya makadirio-Kambi rasmi ya upinzani

Kauli kwenye hotuba hiyo iliyobabisha spika wa bunge asitishe shughuli za leo hadi jioni ilisema, “Tanzania imegeuka chini ya usimamizi wa wizara ya serikali hii ya CCM kuwa taifa linalotoka nyara wanahabari, kuwatesa, kuwangoa kucha na meno, kuwatoboa macho, kuwamwagia tindikali na hata kuwaua.”

Spika amesitisha bunge hilo ili kupata muda wa kuipitia hotuba hiyo kuondoa kauli za uchochezi.

Sikiliza kipande hicho hapa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents